Michezo
Pacquiao na Mayweather wakutana hotelini kuzungumza, ni baada ya kuonana kwenye game ya Miami Heat
Mechi kati ya Manny Pacquiao na Floyd Mayweather huenda ikawepo.
Mashabiki wa ndondi Jumanne hii walijawa na furaha kubwa baada ya kuwaona mabingwa hao wakisalimiana baada ya kukutana kwa mara ya kwanza kwenye game ya Miami Heat.
Kwa mujibu wa mshauri wa Pacquiao, Michael Koncz, Mayweather alienda kwenye chumba cha hoteli cha Pacquiao kuzungumza uwezekano wa pambano lao la May 2.
“Kilikuwa ni kitu kizuri na cha kutia moyo sana, na tunamsifu Floyd kwa kuja,” Koncz aliiambia ESPN.com Jumatano hii.
“Hiyo ni mara ya kwanza wameonana. Nimewahi kukutana na Floyd mara nyingi lakini Manny hakuwahi kupata nafasi ya kukutana naye. Waliongea kwenye halftime, lakini huu ulikuwa mkutano serious na mrefu.”