P-Square ni mashabiki wa ‘Nitampata Wapi’ na Mdogo Mdogo za Diamond
Unataka kuyakuna masikio ya P-Square? Usiimbe kwa kuchanganya na ladha ya Nigeria, imba Bongo Flava halisi! Hilo ndio somo ambalo Diamond amelipata wiki hii kutoka kwa Peter na Paul Okoye.
Msanii wa kundi la P-Square, Peter Okoye akibadilisha mawazo na Diamond Platnumz
Diamond pamoja na wasanii hao nguli wa Afrika na wengine wakiwemo Flavour na Fally Ipupa watatumbuiza leo kwenye tuzo za wanasoka bora wa Afrika wa CAF 2014.
Inadaiwa kuwa baada ya hitmaker huyo wa ‘Number One’ kukutana na Peter, ni yeye (Peter) ndiye aliyeanza kwa kumtambua Chibu na kuanza kuzungumza mawili matatu. Peter anadaiwa kumweleza staa huyo kuwa anamkubali na kama vipi wanaweza kupiga ngoma moja pamoja.
Inabidi tufanya kazi aisee: Diamond na Peter wakibadilisha contacts
Baada ya kukutana na pacha mwingine wa kundi hilo, Paul kwenye hoteli waliyofikia, Paul anadaiwa kumwambia Diamond kuwa anazipenda ngoma zake ‘Ntampata Wapi’ na ‘Mdogo Mdogo’.
Kuna video pia iliyowekwa Instagram inayomuonesha Peter akipiga gitaa na Diamond akiimba freestyle.
Diamond na Fally Ipupa
Chanzo: MillardAyo.com