Ommy Dimpoz amedai kuwa wasanii wengi wamekuwa wakiweka nguvu zao zaidi kwenye video bila kuzingatia nguvu ya audio.
Ameiambia Bongo5 kuwa kwa sasa ubora wa audio ndio kitu anachokipa nafasi zaidi kabla ya kuwazia video yake itakuaje.
“Sasa hivi tunatakiwa tofocus kwenye muziki zaidi, yaani kuutengeneza muziki wenyewe zaidi kuliko kufikiria video,” Ommy ameiambia Bongo5.
“Video hata iwe nzuri vipi, kama nyimbo ni mbaya haiwezi kukusaidia kitu, lazima kwanza tudeal na audio,” amesisitiza hitmaker huyo wa Kajiandae.
“Ukitengeneza mzuri hadi wewe mwenyewe unarelax.”