Burudani

Ommy Dimpoz azungumzia jinsi alivyosherehekea birthday yake mbele ya jukwaa la Fiesta Shinyanga

Ommy Dimpoz ambaye juzi alitimiza miaka kadhaa, alisherehekea siku yake ya kuzaliwa mbele ya mashabiki wa Fiesta wa mkoa wa Shinyanga.

Ommy  akicheza wakati amelala na binti wa Shinyanga
Ommy Dimpoz akicheza wakati amelala na binti wa Shinyanga

Akizungumza na Bongo5 jana wakati akijiandaa kuelekea kwenye tamasha jingine la Fiesta lililofanyika Jumamosi hii mjini Geita, Ommy alisema kuwa ilikuwa surprise kubwa kwake kusherehekea siku yake ya kuzaliwa mbele ya maelfu ya mashabiki wa Fiesta.

“Jana (juzi) nilifanya one of the best shows kwa sababu pia nilikuwa na furaha ya siku ya kuzaliwa kwangu,” alisema. ‘Kwahiyo show ilikuwa nzuri na watu wamejionea hasa Shinyanga jinsi show ilivyokuwa kali.Ilikuwa ni siku kubwa sana katika maisha yangu kwa kusherehekea mbele ya maelfu ya watu.”

“Kile nilichokifanya kwenye show ni kikubwa sana licha ya hivi vingine vya kusema utakata keki na kula lakini kitendo cha kushare birthday na watu kama wale ni kitu kikubwa sana kwangu, vingine nitatoa sadaka kidogo ya kawaida,”alisema Ommy Dimpoz.

Katika hatua nyingine Ommy amewataka mashabiki wake kukaa mkao wa kula kwa video na audio mpya.

“Kuna kazi nyingi zinakuja na kuna kolabo nyingi nimerekodi lakini itakavyokuwa karibuni kutoka watu wataweza kufahamu. Lakini nafikiri mwisho mwa mwezi wa kumi nitarelease video na audio ya wimbo mpya kabisa.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents