Burudani

Ommy Dimpoz awaka, amjibu Nay wa Mitego baada ya kuambiwa ‘Jogoo hawiki’

Msanii wa muziki wa Hip Hop, Nay wa Mitego baada ya kumdiss Ommy Dimpoz kupitia wimbo wake mpya ‘Shika Adabu Yako’, Ommy Dimpoz ameamua kumjibu.
Ommy na Nay

Kupitia wimbo huo, Nay alisema: Huyu jamaa anajiita Dimpoz, Pose kwa Pose, Wanae wanalalamika hawamjui shemeji, Kitaani kuna tetesi mwana hapigi mechi, Mara oh jogoo hawiki, huwa haonyeshi shemeji.

Baada ya kauli hiyo, Ommy Dimpoz kupitia instagram aliandika.

Barua ya wazi kwa Neema wa Mitego kwanza pole kwa Malezi ya Watoto ambao mama zao wamekukimbia, hakuna Mwanamke ambae anaweza kuishi na mwanaume mwenye tabia za kike kama zako ? inatakiwa ujiulize una tatizo gani maana km umaarufu mavi unao,nyumba unayo,magari unayo na hivyo ndo vitu dada zetu wanapenda lakini kwanini wanakukimbia pili kila nikiwaangalia watoto naona kabisa hamjafanana kuna umuhimu wa DNA Da Neema trust me. Hiyo video nimekuwekea hapo juu ni kukuonyesha kuwa mimi na wewe Ligi zetu hazifanani ? vitu navyokula mimi wewe utaishia kuviona kwenye TV maana kuvipata mpaka uwe Unapanda sana Ndege sasa mimi najaza passport ya Tatu wakati wewe hata kurasa 4 za passport yako ya kwanza hujamaliza ? Sasa wewe ushazoea wanawake zako wa jumuiya basi unataka kila mtu apost demu wake haya sasa Chuma hiko kimetoka ulaya kuja kufuata dodoki ??nimekujibu ili nikusaidie promo ya nyimbo yako Atleast upige na Vishoo baba ?? Sema nakuomba usirushe ngumi tu maana nakujua Mzee wa Kupanic Maana katika hao mabebi mama wako kuna mmoja nilishapitaga nae Uliza vizuri atakwambia kama jogoo anawika au vipi ?Ukitaka kudownload wimbo wa @naytrueboy #ShikaAdabuYako nenda kwenye bio ya Da Neema ?

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents