Burudani

Ommy Dimpoz ataja vitu ambavyo muziki wa Uganda ni zaidi ya Tanzania

Kwa mujibu wa Ommy Dimpoz soko la muziki wa Uganda ni imara na linalipa zaidi kuliko la Tanzania.

11424322_478600832313118_777135170_n
Ommy Dimpoz akiwa na msanii wa Uganda, Eddy Kenzo.

Ommy amedai kuwa mwaliko wake wa kwenda kutumbuiza kwenye show kubwa ya mshindi wa tuzo za BET mwaka huu, Eddy Kenzo kumemfumbua macho. Amedai kuwa wasanii wa Uganda wanapata support kubwa kutoka kwa makampuni na mashabiki kuliko wasanii wa Tanzania.

“Nilichogundua ni kwamba support ni kubwa sana, kuanzia kwa mashabiki mpaka kwa makampuni,” Ommy ameiambia Bongo5.

Akitolea mfano tamasha la Eddy Kenzo, Mbilo Mbilo concert, Ommy amedai kuwa makampuni mengi makubwa yalilidhamini kwa kutoa fedha nyingi na hivyo msanii huyo kuingiza fedha nyingi hata kabla ya show yenyewe.

11410472_102583460096673_952848455_n
Ommy Dimpoz akiwa na msanii wa Kenya, Amani ambao wote walialikwa kwenye show ya Eddy Kenzo

Kingine amedai kuwa tamasha hilo lilifanyika kwa siku tatu mfululizo ndani ya jiji la Kampala lakini kwenye viwanja tofauti na vyote vilijaa.

“Zilifanyika show tatu na zote sold out,” amesema.

Ommy aliyetumbuiza hits zake karibu zote kwenye show hiyo amedai kuwa kilichomvutia kingine ni show hiyo kuanzia mapema na kumalizika mapema tofauti na za hapa kwetu ambazo huisha alfajiri. Amedai kuwa kuwa show ilianza saa tatu usiku na kumazika saa sita usiku.

Eddy Kenzo alitumbuiza kwa live band na Ommy amedai uwezo wa bendi hiyo na vyombo vilivyofungwa ulifanya muziki usikike kama unapigwa kutoka kwenye CD!

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents