Ole Sendeka: Lowassa ni mtu muungwana
Msemaji wa chama cha mapinduzi CCM, Christopher Ole Sendeka amesema Edward Lowassa ni muungwana kwa kusalimiana na Rais Dkt John Magufuli bila kinyongo.
Msemaji mkuu wa chama cha mapinduzi (CCM) Christopher Ole Sendeka
“Namfahamu Lowassa ni muungwana hawezi kuacha kusalimiana kwa kupeana mikono na Rais, wamekutana viongozi, rais na waziri mkuu mstaafu hawawezi kuacha kusalimiana”, alisema Sendeka.
Lowassa ni mjumbe kamati kuu ya CHADEMA aliyechuana na Dk Magufuli katika uchaguzi mkuu 2015 mwaka jana, na juzi walikutana kwa mara ya kwanza na mpinzani wake huyo.
Viongozi hao walikutana katika Jubilee ya miaka 50 ya rais mstaafu Benjamin Mkapa katika kanisa la Mtakatifu Petro, lililopo Oysterbay jijini Dar es Salaam.
CHANZO: MWANANCHI
BY: EMMY MWAIPOPO