Burudani
Nisher ataja pesa aliyolipwa kama director kwenye video ya kwanza kutengeneza
Kila kitu kikubwa huanzia kwenye hatua ya chini, kama ni msanii basi lazima utakuta wakati anaanza alifanya show nyingi za bure, kama ni producer wa muziki basi utakuta ametenegezea wasanii wengi mastaa nyimbo bure ili ajitangaze.
Safari ya director wa video Nisher kutoka Arusha pia ilianzia katika hatua za kufanya video bure hadi sasa amefikia hatua ya kutoza milioni tano na zaidi kwa video moja.
Nisher ametaja pesa ya kwanza kulipwa na msanii kama director,
“Kazi Yangu ya Kwanza Kabisa Kuongoza Music Video Iliyonipa Fedha, Nilipata Shilingi 200,000tshs (LAKI MBILI). Kabla ya hapo Nilifanya Video Nyingi Bure, ila hazikufika kokote… #KAMA_ULIKUA_HUJUI_SASA_UNAJUA”. Ameandika Nisher.