Ninaipenda Tanzania daima – Davido
Kwa Davido, Tanzania itaendelea kukaa katika nafasi muhimu sana moyoni mwake. Katika wakati ambao wengi tunadhani ameisahau, hitmaker huyo wa How Long, ameibuka na kuthibitisha kuwa bado ana mapenzi tele na ya milele kwa nchi ya Magufuli.
Ameufungua moyo wake kwenye post ya Diamond katika mtandao wa Instagram ya show yake ya mjini Harare nchini Zimbabwe – Watora Mari iliyofanyika mwishoni mwa wiki.
Kwenye post hiyo ya show hiyo iliyofana na kushuhudia akiujaza ukumbi mkubwa wa HICC akiwa na mwenyeji wake Jah Prayzah, Diamond aliandika:
This Song Called #NumberOneRemix it has more than 18.5 Million Views on Youtube….. Go watch it and enjoy the Mix of Bongo flavour and Naija.”
Post hiyo ilimkuna Davido aliyeandika na kujibiwa na Diamond kama inavyoonekana hapo chini:
Kama ambavyo Jah Prayzah anamshukuru Diamond kwa kumtambulisha kwenye ramani ya muziki wa Afrika, Diamond atamshumkuru milele Davido kwa kumpa shavu kwenye remix ya Number One iliyompa staa huyo wa Tanzania umaarufu mkubwa.