Nikki wa pili afanya collabo ya wasanii sita, Vanessa Mdee , Joh Makini, Jux, Nahreel, Aika na G-Nako
Nikki Wa Pili kutoka Weusi ameingia studio kufanya wimbo mpya ambao amewashirikisha wasanii sita.
Wasanii walioshirikishwa kwenye wimbo huo ambao unafaywa kwenye studio ya The Industry ya producer Nahreel, ni Vanessa Mdee , Joh Makini, Jux, Nahreel, Aika na G-Nako.
Kupitia Instagram Aika Marealle wa kundi la Navy Kenzo amerepost picha wakiwa studio na kuandika,
“UNATARAJIA KITU GANI KWENYE HII COLLABORATION YA @nikkwapili FEAT..#Johmakini@gnakowarawara @nahreel & @aikamarealle @Juma_jux &@vanessamdee ??? #TheIndustrySelfies “
Nikki Wa Pili naye aliandika,
“Hatutengenezi mziki sasa tunatengeneza familia ya mziki mzuri….weusi..v money, jux, aika, nahreel……kwenye track moja kwa hisani ya the industry……utaipata next…..bt do u wana be a lucky fun to have it exclusively??????”