Burudani

Nick wa Pili: Endorsements hazihitaji kuombwa,ni uzuri tu wa kazi zako

Kundi la Weusi limeuanza mwaka 2017 vizuri baada ya wasanii wa kundi hilo wote kusainiwa kuwa mabalozi wa Airtel Tanzania.

Wengi tunaamini kuwa ili msanii awe ‘endorsed’ na kampuni yoyote ni lazima aombe,suala ambalo limekanushwa na muongeaji wa kundi la Weusi, Nick wa Pili.

Kwenye mahojiano na Prince Ramalove kupitia Kings FM, Nick amedai kuwa msanii huitaji kuomba makampuni yakutumie kama balozi wao bali ni uzuri tu wa kazi yako ndiyo utafanya wao wavutiwe na wewe.

“Endorsement sio kitu unaplan,unafanya kazi then kama kazi yako itavutia makampuni,basi utapata kazi,” amesema Nick. Pia Nick ameongeza kuwa producer Luffa ambaye ametengeneza ngoma ya Sweet Mangi ambayo Nick anaitumia kwenye dili hilo, hana asilimia zozote za faida ya dili hilo kwani walishamalizana.

By Prince Ramalove
Kings Fm

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents