BurudaniDiamond Platnumz

Ni kweli Mwana FA na Diamond haziivi kisa Alikiba? FA aueleza ukweli (Exclusive Audio)

Weekend hii kwenye show ya uzinduzi wa Tigo Music iliyofanyika Leaders Club jijini Dar es Salaam, kulienea taarifa kutoka kwa mmoja wa mameneja wa Diamond Platnumz kuwa Alikiba aliwazuia Mwana FA na Shaa kusaliamiana na hitmaker huyo wa ‘Ntampata Wapi’.

10945693_10152967394931001_8126682426113130834_n

Ni kweli?

“Sijui nikwambie nini, lakini kama sitaki kulifanya hili suala liwe habari, kiukweli yaani,” FA ameiambia Bongo5.

Vipi kuhusu uhusiano wake na Diamond baada ya kumshirikisha Alikiba kwenye hit single yake, Kiboko Yangu?

“No we are very good as a matter of fact,! amesema Binamu.

“He texts me (Diamond) every now and then, hivyo namcheck nini. Mameneja wake wote watatu washkaji zangu kinoma na yeye tuna mazoea ya kutosha tu hivi tumekaa one of these days tukapiga story sana, hakuna chochote kilichoharibika,” ameongeza rapper huyo.

“I don’t even think Kiba anamind hiyo na anajua kuwa mimi na Diamond we cool na watu wa Diamond pia we cool, they are cool with me na as a matter of fact wananitaniaga ‘wewe team Kiba wewe’. So we good like that.”

Msikilize Mwana FA akiongea hapo chini.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents