Ni harusi ama video? Picha za ndoa ya kifahari ya Akothee zawaacha mashabiki njia panda!
Unakumbuka kipindi Jaguar alivyodaiwa kufunga ndoa kimya kimya baada ya picha zake kusambaa mtandaoni akibadilishana viapo na msichana mrembo lakini ikaja kubainika kuwa ilikuwa ni video ya wimbo wake One Centimeter?
Akothee akiwa kwenye kile kinachoonekana kama harusi na hivyo kuzua maswali mengi kwa mashabiki wake
Unakumbuka jinsi watu walivyodhani kuwa Ommy Dimpoz amemchukua ex wa swahiba yake, Diamond, Wema Sepetu baada ya kusambaa picha za utata za wawili hao lakini kumbe ikaja kubainika kuwa ni Wema ni Wanjera kwenye video ya Ommy ya wimbo wake mpya?
Na sasa ni zamu ya Akothee, msanii wa Kenya anayefahamika kwa utajiri wake! Muimbaji huyo amewaacha watu njia panda baada ya kushare picha akionekana kufunga ndoa ya kifahari mbele ya umati mkubwa wa watu wenye mchanganyiko wa rangi mbalimbali.
Mashabiki wake kwenye Facebook wanaendelea kumpongeza kwa kuolewa.
“Real friends for life thanks once again for attending my wedding,” ameandika Akothee. Jionee picha za harusi hiyo pamoja na zingine anazoonekana muimbaji huyo na mume wake mpya!