Burudani

Ni AY ndiye aliyenibakisha kwenye tasnia ya burudani, nilikuwa bandarini huko – Sallam

Meneja wa WCB ya Diamond Platnumz ambaye pia ni meneja wa AY, Sallam SK aka ‘Fundi Mitambo’ amefunguka kwa kudai kuwa alitambulishwa na rapper AY kwenye tasnia ya burudani.

Sallam ambaye ameonyesha uwezo mkubwa katika jukumu la kumsimamia Diamond, alikuwa akijihusisha na biashara ya magari bandarini.

“Ni AY ndiye aliyenibakisha kwenye tasnia ya Burudani nilikuwa zangu huko bandarini na shughuli zangu huko,” Sallam alikiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM.

Mapema mwaka 2016 Sallam alieleza furaha yake ya kufanya kazi na legendary ‘AY’ katika ukurasa wake wa Instagram huku AY akitupia comments zake juu ya meneja huyo mpya.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents