BurudaniMuziki

New Music: Mbunge Ester Bulaya aijibu ngoma ya Ben Pol ‘Phone’, atumia ushairi na kuingia studio

Mbunge wa Bunda Mjini, Ester Bulaya ameonesha upande mwingine nje ya uwezo wake katika siasa. Mheshimiwa Bulaya ni malenga wa kutisha na kuonesha kuwa yupo vizuri, ameijibu ngoma ya Ben Pol, Phone.

Haijaishia tu kuandika mashairi, bali ameingia booth kwenye studio za Tiddy Hotter na kuyarekodi kwenye mdundo.

“Alinicheki akaniambia anapenda nyimbo zangu na hii Phone imembamba lakini ameandika kitu anataka nimpe msanii yoyote wa kike aiimbe,” Ben ameiambia Bongo5. “Nikamuomba arekodi yeye hata kama sio muimbaji basi aijibu kwa ushairi, akakubali.”

Msikilize na yasome maishari hapo chini.

Umesema nisishike simu yako,
Nisishike mpenzi wako,
Kipi siri yako, hasa ufichacho ?

Lazima niishike, mimi mpenzi wako,
Napaswa nijiridhishe, kipi ukilindacho?
Simu uitumiapo, hiyo si mboni yako,

Kwa sasa ni wapenzi,
ndio maana waniita baby,
Wapaswa kuwa wazi, kwangu si kwa aziz,

Sina mwingine mpenzi, ni wewe laaziz,
Lazima nilinde penzi, lisidokolewe na wezi,
Wewe ni wangu mwenzi, wivu hapa makazi,

Ninapoishika simu, ni faida ya mapenzi,
Nikijua kuna sumu, ihusuyo wavamizi,
Lazima nipate hamu, na kuweka vizuizi,

Nikishamjua mwizi, siwezi kukuacha,
Nitampa na ulinzi, penzi halitachacha,
Mwenye wazimu na penzi, simu hawezi acha,

Anayempenda wake, simu huchunguza,
Atavilinda vyake, vya simu huchombeza,
Na hiyo ni kazi yake, hapaswi kuchokozwa,

Mpende akiishika, simu yako ni yake,
Hupaswi kukasirika, umeuteka moyo wake,
Usione patashika, hayo majukumu yake,
Baby simu kuishika, ndiyo ulinzi wake,

Hakushikii mtutu, na silaha ya moto,
Anashikilia simu, penzi liwe motomoto,
Wapaswa kuwa muaminifu, hiyo si ngoma ya kitoto.

SHAIRI – MH. ESTER BULAYA (MBUNGE – BUNDA MJINI)

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents