Ne-Yo akikubali kipaji cha uchoraji cha Mtanzania huyu, aipost picha yake kwenye Instagram
Chrissy Renny ni kijana mwenye kipaji kisicho cha kawaida – anachora picha kwa kutumia kalamu ya wino ambayo ukiilinganisha na picha original, unaweza kudhani aliyochora ni photocopy.
Picha ya Ne-Yo iliyochorwa kwa mkono kutumia kalamu ya wino
Cha kufurahisha zaidi, Chrissy ni Mtanzania na sasa jina lake limefika Marekani – thanks kwa shavu alilopewa na Ne-Yo.
Chrissy ambaye huchora picha za mastaa anaowapenda na kuziweka kwenye akaunti yake ya Instagram, alimsurprise Ne-Yo aliyekuwa nchini Afrika Kusini wiki iliyopita kwenye MTV MAMA, kwa kuchora picha yake.
“A pen drawing of Ne-yo can’t wait for his performance on #mtvmama today 18 july, #nonfiction2015 #neyonation #neyo please tag him too @neyo, aliandika Chrissy kwenye picha hiyo.
Ne-Yo ameipenda picha hiyo na hakusika kuipost kwenye akaunti yake yenye followers milioni moja na kuandika, “This is dope! Shout out to @chrissrenny #NEYONATION #Art #NONFICTION2015.”
Tangu aanze kuchora picha za mastaa mbalimbali, Ne-Yo ndio msanii wa kwanza wa Marekani aliyeiweka picha hiyo kwenye akaunti yake na ndio maana Chrissy amekipokea kitendo hicho kwa furaha kubwa.
“Am shocked thank you neyo for the appreciation and thanks to everyone for the tags you guys are so dope @neyo @evey1,” aliandika Chriss.
Tayari Chrissy amepata mashabiki duniani kote.
“@neyo liked and shared @chrissrenny …that’s how I came here..love your work. Greetz from The Netherlands,” ameandika msichana mmoja kutoka Uholanzi.
Chini ni baadhi ya picha za mastaa alizochora Chrissy.
Msanii wa tamthilia ya Empire, Taraji P Henson
Linah
Rihanna
Chris Brown
Rihanna
Profesa Jay
Ciara
Yemi Alade