Burudani

Ne-Yo aeleza kwanini alikuwa na hamu ya kuonana na Diamond Platnumz alipoenda Afrika Kusini

Muimbaji wa Marekani, Shaffer Chimere Smith maarufu kama Ne-Yo ameitaja sababu iliyomfanya atake sana kukutana na Diamond Platnumz.

11375363_542992865841404_1240496137_n

“Baada ya watu kusikia kuwa nilikuwa nakuja kwenye MAMAs jina pekee ambalo walikuwa wakilitaja kwangu ni Diamond Platnumz,” Ne-Yo alimwambia Vanessa Mdee kwenye interview ya MTV Base.

“Nikasema ni lazima nikutane na huyu jamaa, nahitaji kumuona,” aliongeza.

Siku moja kabla ya tuzo hizo pia, Diamond alielezea jinsi Ne-Yo alivyomtafuta. “Wakati nazungumza na D’banj @salaam_sk alinifata na kuniambia @neyo anakutafuta anataka kukuona…” Ungependa kujua kilichofata??? Kaa karibu na TV, Radio yaani Kiufupi Media zako Soon utayaskia,” aliandika Diamond kwenye Instagram.

Ne-Yo na Diamond ni miongoni mwa wasanii waliotumbuiza kwenye MTV MAMA 2015.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents