Burudani

Nay wa Mitego na Professor J ni miongoni mwa wasanii wanaoleta wimbo kukaguliwa kabla ya kuzitoa – BASATA

Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) limewataka wasanii wa muziki nchini kufuata taratibu za kupeleka nyimbo zao kukaguliwa kabla hazijatoka ili kuondoa usumbufu ambao umekuwa ukijitokeza mara kwa mara kwa baadhi ya wasanii ambao wamekuwa wakitoa nyimbo bila kukaguliwa na baadaye kufungiwa na baraza hilo kutokana na kukosa maadili.

Hayo yamesemwa na Afisa habari wa Basata, Agnes Kimwaga alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika semima maalum ya mazunzo juu kutambua shughuli mbalimbali zinazofanya na baraza hiyo.

Alisema wasanii wote wanatakiwa kuwasilisha kazi zao Basata ili zikaguliwe kabla ya kutoka na pia kushauriana namna nzuri ya kuufikisha ujumbe wao kwa jamii bila kuvunja utaratibu.

“Mpaka sasa wasanii ambao wanaleta kazi zao kukagulia ni Nay wa Mitego tena baada ya kupata misukosuko lakini kwa sasa kabla ya kutoa kazi analeta ikagulie, pia na Professor analetaga,” alisema Kimwaga.

Aidha alisema baraza hilo lipo kwajili ya wasanii hivyo wasanii wanatakiwa kulitumia ili kustawisha sanaa ya muziki nchini.

Pia alisema Baraza hili linatoa msaada wa kisheria pamoja na wakibishara kwa wasanii ambao watahitaji.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents