Burudani

Nay wa Mitego aijibu diss ya Madee kwenye ‘Hela’, auita wimbo mbaya kuliko mbaya za mwaka huu

Wafalme wa Manzese, Madee na Nay wa Mitego, wameirejesha tena bifu yao.

Imerudi upya baada ya Madee kuandika mstari kwenye wimbo wake mpya, Hela ambao umetafsiriwa kumwendea hasimu wake, Nay.

https://www.youtube.com/watch?v=rHeRynQMB-Q

“Yule kijana wa home sio staa, anatukana hata waliomzaa, wivu tamaa na njaa ukiendekeza ujue kidole utakaa,” Madee amerap kwenye wimbo huo.

Baada ya muda mfupi tangu wimbo huo utoke, Nay aliandika kwenye Instagram, “Leo nimesikia Wimbo Mbayaaaaa kuliko nyimbo mbaya nilizowahi kusikia Mwaka huu.”

“Mtag uyo Msanii mwenye huo wimbo Kama ushausikia..?!”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents