Burudani

Baby J akanusha kuwa mjamzito

Mwanadada anayefanya muziki wa Bongo Fleva akiwakilisha visiwa vya Zanzibar Baby J amekanusha tetesi zilizoenea kuwa ni mjamzito.

Baby J

Baby J ambaye muda mwingi yupo maskani yake Zanzibar ameimbia Bongo5 kuwa ukimya wake ndiyo umesababisha watu kuhusi kuwa ni mjamzito

“Unajua kweli nimekuwa kimya lakini ni mipango naweka sawa na pia nilikuwa na mambo yangu ya kifamilia zaidi,” amesema. “Ila nashangaa watu kusema kuwa mimi ni mjamzito ni kitu ambacho kinanishangaza watu wanajua mie mjamzito wakati hata mimi mwenyewe sijui! Au kwakuwa wanaona labda nimenenepa ndio maana. Kazi zipo tayari zina subiri kutoka, kwahiyo muda wowote kazi itatoka mashabiki wake tayari tu,” ameongeza.

Hivi karibuni Mkubwa Fella alitangaza kumuongezea Baby J kwenye familia yake ya Mkubwa na Wanawe.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents