Habari

Nampenda Sugu mpaka sijielewi – Faiza Ally

Msanii wa filamu, Faiza Ally wakati inaelekea siku ya birthday ya mtoto wake Sasha, amefunguka na kueleza yamoyoni juu ya baba watoto wake, Mh Joseph Mbilinyi ‘Sugu’.
Sugu na Faiza
Sugu na Faiza kabla hawajaachana

Mwigizaji huyo ambaye anajipanga kuachia filamu yake mpya ‘Baby Mama Drama’ amesema ataendelea kumpenda Mh Sugu kwa kuwa bila yeye asingekuwa mama kwa sasa.

“Nakumbuka 2012 wakati kama huu nilianza kuumwa uchungu wako mwanangu. Yaani nilikua na raha toka siku baba yako aliyoniomba tuzae nilianza kukupenda kabla sijapata mimba. Nilipo pata ndio uwii nilikua natamani siku ifike tuonane mwanangu sasa ndio nika zidi kumpenda baba yako vibaya sana Hahhahahah,” aliandika Faiza Instagram.

“Nakumbuka siku moja na tumbo kubwaa baba yako akaniangalia nilikua na chupi tu hahaha nilikua niko bize nampangia nguo zake kabatini akaniambia sister du nime kukomesha nikamwambia aawapiiii huja nikomesha nafurahi Kila step ya mimba yangu. Sasha Mpenzi wangu stori ni nyingi sana siwezi kumaliza. Kiufupi tu toka Kwenye mimba yako nilikua na furaha sana mpaka siku nilio kupata.Mpaka leo na mahaba ndio yanazidi juu yako mwanangu. Baba yako ndio Kabisa nampenda mpaka sijielewi Kila niki kuangalia najua bila yeye leo hii nisinge kuwa Na furaha hahahahaaa tulishirikiana kitendo tukakupata naachaje kumpenda hehehehee. Asante baba Sasha Kwa kunifanya niwe mama. Mungu akubariki katika Kila unalo fanya uendelee kuwa hai mwanangu aendelee kuwa na baba yake, Asante dogo#asante sugu#Asante Joseph #asante mei Asante baba Sasha … Hatujaonana zaidi ya mwaka#hatuja ongea zaidi ya mwaka lkn haijawahi kupita siku sija kuzungumzia na sijawahi kukuacha kukupenda baby daddy… Nakupenda Leo#kesho Na siku zote ????. Sasha birthdays loading,” alifafanua zaidi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents