Kama kuna ukurasa katika kitabu cha maisha ya Lulu Diva ambao angeweza kuufuta, ni ule wa kufanya kazi kama mrembo kwenye video za Bongo Flava.
Lulu ameiambia Bongo5 kuwa anajuta kufanya kazi hiyo.
“Kama kuna kitu ambacho najutia kukifanya, ni video vixen,” amesema. “Kitu ambacho mpaka kesho ukiniuliza katika industry ya entertainment ambacho unajuta kukifanya ni nini, mimi sijajutia kuwa miss, lakini video vixen najutia kwasababu wale wanaofanya ile kazi wanajidhalilisha sana, yaani wanajiweka hawana thamani, wanajitoa thamani yao. Kwahiyo hata kama wewe utakuwa unajiweka tofauti, sababu wenzako washafanya hivyo na samaki mmoja akioza ni wote, mnaonekana wote mko hivyo,” ameongeza.
Nilipomuuliza kama akilipwa fedha nyingi kuonekana kwenye video, jibu lake lilikuwa ni, “Siwezi kukubali, sasa hivi mimi naconcentrate na muziki wangu.”
Lulu ataachia kazi yake mpya, Usimwache Jumamosi hii.