Habari
Naj: Sipendi mwanaume anayependa soka
Kama wewe ni mwanaume na ni shabiki wa ligi ya England, ligi kuu ya Tanzania au zingine jipange kwasababu umepoteza kigezo cha kumfanya Naj akuite mpenzi wake.
Muimbaji huyo wa ‘Don’t Let Me Go’ hapendi mwanaume anayependa soka.
“Sasa hivi siwezi kumdate a guy who likes football,” Naj alisema kwenye kipindi cha Chill na Sky.
“Sio type yangu cause they are so much into other guys in shorts running around for 90 minutes kicking balls halafu mwisho wa siku wanafunga magoli mawili,” aliongeza.
“We wasted 90 minutes mtu mwenyewe ameenda kufunga magoli mawili, that’s a waste of my time, we could have done so much.”
Naj amesema anachopenda zaidi ni kuangalia movie. Sikiliza kipindi chote hapo chini.