Michezo

Nahodha wa Bafana Bafana Senzo Meyiwa aliuawa akimuokoa mpenzi wake

Nahodha wa Bafana Bafana na Orlando Pirates Senzo Meyiwa aliuwa kwa risasi na majambazi alipokuwa akijaribu kumlinda mpenzi wake walipokuwa nyumbani kwa mpenzi wake huyo, karibu na Johannesburg, maofisa wamesema leo.

10707195_719538581468408_232896984_n
Senzo na mpenzi wake Kelly Khumalo

Mlinda mlango huyo wa Orlando Pirates aliuawa jana baada ya kupigwa risasi kifuani mbele ya mpenzi wake ambaye ni muimbaji na muigizaji. Katika tukio hilo, watu wawili waliivamia nyumba hiyo liyopo katika mji wa Vosloorus na kutaka wapewe simu, fedha na mali zingine.

10747873_808233495894531_619749870_n
Hii ni picha ambayo Kelly aliiweka kwenye akaunti yake ya Instagram, Jumapili, masaa kadhaa kabla ya Senzo (kushoto) kuuawa

“Senzo alitaka kumlinda Kelly sababu mmoja wao alikuwa amemwelekezea bunduki,” afisa mmoja aliwaambia waandishi wa habari. Polisi wanadai kuwa siku ya jana watu watu wawili waliingia nyumbani kwa Khumalo saa mbili usiku huku mwingine akisubiri nje na walipomaliza walikimbia.

Orlando Pirates,  imeandika kwenye Twitter: “@Orlando-Pirates family has learned with sadness of the untimely death of our number 1 keeper & captain Senzo Meyiwa.”

Irvin Khoza, mwenyekiti wa club hiyo ameongeza: “This is a sad loss to Senzo’s family especially his children, to Orlando Pirates & the nation.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents