Habari

Mzee Upako awachimba mkwara wanaodai anatumia ulabu

Baada ya hivi karibuni kuenea habari kuwa mchungaji wa kanisa la Maombezi, Anthony Lusekelo amemfanyia fujo jirani yake hivyo kushikiliwa na polisi na kwamba alionekana akiwa amelewa pombe, ameibuka na kuwaonya wale wanaozusha habari za uongo.

mzee-wa-upako3

Akiwahubiria waumini wake Jumapili hii, Mchungaji huyo alisema, “Wiki iliyopita nilikuwa wizara ya mambo ya ndani, baadhi ya maofisa wakaniona, wewe mzee wa upako, wewe mzee wa upako, askari mmoja akaniuliza unachukua sadaka unaenda kunywa pombe. Nikawauliza hiyo pombe nilikunywa wapi, halafu pombe zipo nyingi, taja ni pombe gani, ukienda mbali zaidi ungeuliza nililewa nini, maana hata upako wa roho mtakatifu ni ulevi.”

Mchungaji huyo aliongeza kuwa hakuna binadamu atakayeweza kumwangusha kwa kipawa na karama aliyopewa na Mungu.

BY: EMMY MWAIPOPO

CHANZO: MWANANCHI

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents