Habari

Mwanamke ambaye ni mkongwe zaidi duniani afariki New York

Mwanamke aliyetambuliwa kuwa mkongwe zaidi duniani amefariki dunia alipo kuwa akitibiwa jijini New York, Marekani, madaktari wamesema.

160513080207_susannah_mushatt_jones_640x360_reuters_nocredit
Bi Jones alizaliwa mwaka 1899

Susannah Mushatt Jones, amefariki akiwa na umri wa miaka 116.

Alizaliwa eneo la mashambani jimbo la Alabama mwaka 1899, na amekuwa akiugua kwa siku kadha.

Mwanamke Mwitaliano, Emma Morano, ambaye ni mdogo wa umri wa Bi Jones kwa miezi kadha, sasa ndiye anayetambuliwa kuwa mwanamke mkongwe zaidi duniani.

150707082109_mushatt_624x351_ap
Morano sasa ndiye mwanamke mzee zaidi duniani

Anaaminika kuwa mtu pekee duniani aliyezaliwa karne ya 19 ambaye bado yuko hai.

Source: BBC

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents