Burudani

Mwana FA hana mpango wa kufanya kazi na wasanii hawa

Mwana FA amewataja wasanii ambao hana mpango wa kufanya nao kazi kwa sasa.

Hitmaker huyo wa Dume Suruali, amekiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio Jumanne hii kuwa kwa sasa hana mpango wa kufanya kazi na Lady Jaydee, Prof Jay, Juma Nature.

“Kwa sasa sina mpango wa kufanya kazi na Lady Jaydee, harafu hili swali limekuwa likijirudia sana sina mpango wa kufanya kazi na Prof Jay, Juma Nature na wasanii wengine wengi. Lakini sina tatizo nao na wala sina tatizo na yoyote kati yao.”

Rapper huyo ameongeza kuwa kwa sasa muziki wa Hip Hop unafanya vizuri na hii ni kutokana na wasanii wa muziki huo kugundua sehemu waliyokuwa wakikosea.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents