Mwana FA aungana na Jay-Z, Beyonce, Rihanna kwenye NBA All-Star Game (Picha)
Jumapili ya jana Mwana FA aliungana na mastaa wengine wa Marekani wakiwemo Jay Z na Beyonce pamoja na rais wa zamani wa Marekani, Bill Clinton kwenye NBA All-Star Game katika uwanja wa Madison Square Garden jijini New York Marekani.
Mwana FA akiwa kwenye uwanja wa Madison Square Garden, New York
Mwana FA ameiambia Bongo5 kuwa All-Star Game ni noma.
“Unajua ni kama mchanganyiko wa NBA nzima na top artists kibao, ni
event kubwa. I saw Nas performing, we mtu wa hip hop unajua what that means,” amesema Mwana FA.
Picha ya tiketi ambazo Mwana FA alitumia kuingilia kwenye michezo hiyo. Tiketi moja ni $350 (takriban shilingi laki sita za Tanzania)
Russell Westbrook wa timu ya mastaa wote wa Western Conference, akikabidhiwa tuzo ya NBA All-Star Game MVP trophy kwenye michezo hiyo ya 64 ya NBA All-Star Game, February 15, 2015, Madison Square Garden New York
Rihanna pia alihudhuria
Tazama picha zaidi za mastaa hao.