Bongo Movie
Muigizaji Mzee Manento amefariki dunia
Muigizaji wa filamu Mzee Manento aliyewahi kuigiza filamu kama Hero of the church, Dar to Lagos na Fake Pastor amefariki dunia jana
Mzee Chilo ameiambia Bongo5 kuwa amepokea taarifa za kufariki kwa msanii huyo.
“Hata mimi nimepata taarifa hizo, lakini sijajua msiba upo wapi na mimi ndo nataka kuanza kufuatilia, kweli amefariki, ni mkristo kwahiyo nadhani hawawezi zika mapema hii. Nimesikia amefia katika hospitali na TMJ,” amesema Mzee Chilo.