Mtoto wa Diddy aachia nyimbo zake mbili kwa pamoja
Baada ya kusaini kwenye lebo ya Bad Boy miezi kadhaa iliyopita mtoto wa Diddy, rapper Christian Combs ameachia nyimbo mbili chini ya lebo hiyo.
Christian Combs alisaini kwenye lebo hiyo inayomilikiwa na baba yake [Diddy] mwezi April mwaka huu na sasa ameachia nyimbo mbili, ikiwemo ‘Party’ aliyowashirikisha member kutoka kwenye lebo hiyo, SNL and CYN huku wimbo huo akiwa amecopy melody kutoka kwenye wimbo wa ‘Party Ain’t a Party’ na wimbo mwingine wa ‘One for Me’.
Baada ya kuachia nyimbo hizo kutokana na furaha aliyokuwa nayo, Diddy kupitia akaunti yake ya instagram aliandika, “WORLD PREMIERE!! New music from my son @Kingcombs on @HotNewHipHop RIGHT NOW!!! Link in my bio!! Let’s GO!! #Party #OneForMe #CYN”
Aidha Christian Combs anatumia jina la King Comb kama ndiyo jina lake la usanii.