Habari

Mtangazaji wa Clouds FM Da’Huu asherehekea siku ya kuzaliwa kwa kutoa msaada Amana

Mtangazi wa Clouds FM kupitia kipindi cha Leo Tena, Husna Abdul aka Da’Huu akiambana wa wasanii wa muziki ameshereekea siku yake ya kuzaliwa weekend hii katika hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam kwa kutoa msaada wa vitu mbalimbali.

IMG_9893

Husna Abdul ambaye pia ameteuliwa kuwa BALOZI WA KUJITOLEA WA WATOTO katika hospitali hiyo, aliambatana na wafanyakazi wa Clouds FM, wasanii wa muziki, wadau na wasikilizaji wa kituo hicho cha redio.

Shilole na Dahuu wakiwa ndani ya hospital ya Amana wodi ya watoto
Shilole na Da’huu wakiwa ndani ya hospitali ya Amana wodi ya watoto

Husna alitoa misaada ya vifaa tiba katika wodi ya wazazi katika hospitali hiyo ya Amana, kama sehemu ya maadhimisho ya siku yake ya kuzaliwa.

Kwa upande wake Husna Abdul alisema ameamua kufanya hivyo ili kuwasukuma watu wengine kukumbuka mahali ambapo walikozaliwa kuliko kupoteza pesa kufanya sherehe kubwa huku wakati huo huo kuna watu wanaojifungua kwa shida vifaa vya uzazi hakuna, hivyo kuwapa chagamoto wengine walione hilo.

Aidha kwa kupitia mwakilishi wa Mganga Mkuu wa hospitali ya Amana, Bi Getruda Masawe, alimshukuru Husna Abdul na Clouds kwa ujumla kwa kuwapatia misaada ya vifaa tiba hospitalini hapo na kuwaomba wengine waige mfano wa Balozi wa Watoto hospitalini hapo, Husna Abdul.

Mtangazi wa Leo Tena ya Clouds Fm, Dahuu
Mtangazaji wa Leo Tena ya Clouds Fm, Da’Huu


Shilole akizungumza na waandishi
Shilole akizungumza na waandishi

IMG_9877 - Copy

IMG_9891 - Copy

IMG_9899 - Copy

IMG_9899

IMG_9954

IMG_9962

IMG_9964 - Copy

IMG_9974

IMG_9979 - Copy

IMG_9988 - Copy

Related Articles

Leave a Reply

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents