Burudani
Msechu: Ukubwa wa Nyota unanipa wakati mgumu kuja na ngoma ya kuizidi
Peter Msechu amesema kwa jinsi wimbo wake Nyota ulivyofanya vizuri, anashindwa kupata wimbo mwingune utakaoweza kufanya vizuri zaidi yake.
Msechu ameiambia Bongo5 jana kuwa licha ya kuwa tayari ana nyimbo nyingi amerekodi, anaona hazina nguvu kama Nyota iliyotangulia.
“Sasa nipo kwenye maandalizi ya video mpya pia nina kazi nyingi ambazo zipo tayari lakini napata wakati mgumu kupata wimbo ambao utau-replace Nyota,” amesema. “Tayari ni nyimbo nyingi nimerekodi lakini naona bado.”
“Kazi zipo nyingi sana, ila ukipita uchaguzi ndio nitajua sasa naachia ngoma gani katika nilizonazo.”