Msanii wa Nigeria Burna Boy aponda mfumo wa muziki wa Nigeria, adai umejaa siasa
Muimbaji wa Dancehall kutoka Nigeria, Burna Boy ameponda mfumo wa muziki wa Nigeria na kudai kuwa umejaa siasa ndio sababu hapati tuzo nyingi anazostahili.
Akizungumza na jarida la Fader, Burna amesema kutokana na hayo anajiona kama yeye si sehemu ya muziki wa Nigeria kwasababu kuna baadhi ya watu walioutawala muziki huo wasiompenda.
“Kusema kweli ni siasa tupu, sijioni kama ni sehemu ya kiwanda cha muziki, angalia tuzo, sipati tuzo kwasababu wanaoutawala hawanipendi, mimi sio kama wengine, siwezi kufanya kama wafanyavyo wengine, hawapendi hicho”.
Muimbaji huyo wa ‘Check and Balance’ ameongeza kuwa licha ya kuwa hana wafuasi wengi Instagram na Twitter lakini anaamini anafanya vitu vizuri na vikubwa kuwazidi wasanii wengine wenye wafuasi wengi kwenye mitandao ya kijamii.