Burudani

Mr T Touch asema hajaachana vibaya na Nay wa Mitego ‘nimeamua kutetea maisha yangu’

Mtayarishaji wa zamani wa studio ya Nay wa Mitego ‘Free Nation’ Mr T Touch amefunguka na kuzungumzia mahusiano yake na aliyekuwa bosi wake baada ya wawili hao kudaiwa kuachana vibaya.

13736136_1027734437295098_733240745_n
Mr T Touch akiwa ndani ya studio yake mpya

Akiongea na Bongo5 Jumanne hii, Mr T Touch amesema ameachana na Nay wa Mitego ili kutengeneza maisha yake binafsi.

“Hakuna ugomvi wowote ila mimi nimeamua kufanya maisha yangu ambayo nahisi ni bora kwangu kwa sababu sisi ni binadamu na kila kwenye mwanzo kuna mwisho ,” alisema T. “Kwa hiyo ni vitu vya kawaida mimi nimetoka Free Nation sio kwa bifu lakini ni kujitetea kwenye maisha yangu, kwa hiyo nimefungua studio mpya na nimewekeza pesa nyingi kwa sababu studio ndio maisha yangu,”

Pia mtayarishaji huyo amesema atafanya kazi na Nay wa Mitego kwa vigezo maalum tofauti na mwazo.

“Siwezi kukataa kufanya kazi na Nay wa Mitego, kama akija tutasaini mkataba alafu kazi itafanyika lakini sio kama zamani hii ni kibiashara zaidi,” alisema Mr T Touch

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents