Moze Radio na Weasle ndani ya Maisha!!
Kundi la wasanii kutoka Uganda leo wanatarajia kufanya shoo usiku katika Ukumbi wa Maisha Club, Penniel Mungilwa afisa habari wa Maisha Club aliongea na waashindi wa habari na kuwatambulisha wasanii hao kutoka Uganda.
Penniel alisema kuwa kila Ijumaa ya mwisho wa mwezi watakuwa wanaleta wasanii kutoka nje ya nchi, na hajalisha ni nchi za Afrika tu hapana, msanii kutoka nchii yoyote duniani.
Penniel alisema wameanza programu zoezi hili toka mwezi uliopita na wataendelea kufanya hivyo kwa lengo la kuwaburudisha na kuwafurahisha washabiki wa Maisha Club, ikiwa na kiingilio kiingilio kilekile.
Weasle na Moze Radio wamesema kuwa leo usiku tunatrajia kufanya tutafanya shoo ya ukweli.Wasanii hawa wanatamba na nyimbo kama Nakudata, Zuena pamoja na Breadad Bata.
Shoo hiyo imedhaminiwa na Air Uganda , DST pamoja na Class FM.