Bongo Movie
Monalisa, Riyama, Wastara na Claud kwenda Uingereza kufanya filamu iitwayo ‘Ughaibuni’
Waigizaji wanne wa Tanzania ambao ni pamoja na Monalisa, Riyama Ally, Wastara Juma na Claud, Jumatano hii wanatarajia kusafiri kuelekea jijini London, Uingereza kufanya filamu iliyopewa jina la ‘Ughaibuni’.
Wasanii hao wanatarajia kwenda kukaa nchini humo kwa wiki mbili ama tatu. Filamu hiyo imeandikwa na kudhaminiwa na kampuni ya Didas Entertainment ya jijini London inayohusika na masuala ya burudani.