Burudani

Mimi ni mwanamke – Baba wa Kim Kardashian, Bruce Jenner (Video)

Baba wa kambo wa Kim Kardashian, Bruce Jenner ameweka wazi kwa mara ya kwanza uamuzi wa kujibadilisha kuwa mwanamke.

Katika mahojiano maalum aliyofanya na kituo cha runinga cha ABC News, Kris alisema kwa miaka yote amekuwa akiishi kama mwanamke zaidi ya muonekano wake wa kiume.

Kwenye mahojiano hayo, Bruce alisema alianza kujihisi kuwa na vitu vya kike akiwa bado mdogo na amekuwa akipambana na hali hiyo katika maisha yake yote.

“Ubongo wangu ni wa kike zaidi kuliko wa kiume,” alisema. “Ni ngumu kwa watu kuelewa hilo lakini hivyo ndivyo nafsi yangu ilivyo.”

Jenner ana watoto sita aliowazaa mwenyewe, Burt, Cassandra, Brandon, Brody, Kendall and Kylie na wa kambo ambao ni Kourtney, Kim, Khloe na Rob Kardashian.

Bruce amewaambia watoto wake kuwa wanaweza kuendelea kumuita baba lakini bado hajaweka wazi jina la kike alilochagua kutumia.

Kwa miaka kadhaa amekuwa akifanyiwa upasuaji wa sura na kuwekewa hormone ya kike, estrogen kwa miaka mitano miaka ya 1980s.

Familia yake imeungana mkono na kuahidi kuwa naye bega kwa bega.

Hivi ndivyo wanae wametweet baada ya interview hiyo:

Kim Kardashian: Love is the courage to live the truest, best version of yourself. Bruce is love. I love you Bruce. Your honesty has opened the doors for others to be courageous and live an authentic life! #respect #hero #family

Kourtney Kardashian: Couldn’t be a more proud daughter. With courage and bravery, let’s change the world. I am honored to stand by Bruce’s side and support him.

Khloé Kardashian: Just finished watching the #BruceJennerInterview with the family. Bruzer, I’m soooo proud of you! Dads really are heros ❤️

Kendall Jenners: I love you, So very proud of you, my hero.

Kylie Jenner: Understandingly, this has been very hard for me. You will hear what I have to say when I’m ready to but, this isn’t about me. I’m so proud of you, Dad. You are so brave. My beautiful Hero.

Aliyekuwa mke wake, Kris Jenner ametweet: Not only was I able to call him my husband for 25 years and father of my children, I am now able to call him my hero.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents