Burudani
Mike Tee aibiwa baada ya kuvamiwa na watu wenye silaha
Msanii wa Hip Hop ma muongozaji wa video, Mike Tee aka Mnyalu leo asubuhi ameibiwa laptop pamoja na vifaa vingine baada ya kuvamiwa na watu wenye silaha wakati akielekea kazini.
“Leo hii asubuhi majira ya saa 05:30 nikiwa naelekea ofisini , nimevamiwa na watu watano wenye mapanga wakiwa na gari aina RAV4 ya silver no. T280AZQ wamechukua laptop yangu MacPro, External HDD 4, Headphones za Sony na Modem. Ninachoshukuru nimepona ila nnachoomba atakayeiona gari hii popote atutaarifu kwa number +255754310202 / na ntampatia cash 300,000 then ntadeal nao mwenyewe,” aliandika kwenye ukurasa wake wa Facebok.