Burudani
Mike T aelezea hatua iliyofikiwa baada ya kuibiwa baadhi ya mali zake
Mike Tee amefanikiwa kupata ‘clue’ itakayomwezesha kujua ukweli kufuatia kuibiwa baadhi ya mali zake.
Kwenye tukio hilo, Mike Tee aliibiwa laptop, simu, pamoja na vitu vingine.
“Nashukuru wote kwa kujilia hali na kunipa pole. Nashukuru polisi nimekwenda jana na baada ya kureport, tumefungua jarada cha kuchekesha baada ya kufuatilia number zilizofungwa kwenye ile rav4 ni za Mitsubishi canter ya bakhresa. Kifupi number fake zimetumika. Ila nnachoshukuru nimepewa mtonyo sinema yangu kwao itakuwa balaa, gari imejulikana,” ameandika kwenye Facebook.