Habari
Mgao wa Umeme: Tanzania yaingia gizani kwa siku 10
Kuanzia Jumamosi hii, mikoa mingi nchini imeingia kwenye mgao wa umeme wa siku 10. Mgao huo wa umeme unatokana na kuzimwa kwa mitambo ya kampuni ya Pan African iliyopo Songosongo.
Mitambo hiyo inazimwa kwa sababu ya matengenezo ambayo Tanesco imesema ni ya lazima kwakuwa kutakuwa na upungufu mkubwa wa umeme kwenye gridi ya taifa.