Burudani
Mfahamu Miss Universe Iris Mittenaere kupitia picha hizi 10
Jina la Iris Mittenaere lilianza kuwa maarufu duniani kuanzia usiku wa Jumapili ya Januari 30 pale aliposhinda taji la Miss Universe, shindano lililofanyika jijini Manila, Ufilipino baada ya kuwabwaga washiriki wengine 85.
Iris ambaye pia ndiye mshindi wa taji la Miss Ufaransa 2016 amekuwa mrembo wa pili kutoka Ufaransa kushinda taji hilo baada ya Christiane Martel ambaye alishinda taji hilo mwaka 1953. Hizi ni picha 10 za mrembo huyo tumekuandalia kutoka katika mtandao wake wa Instagram ili uweze kumfahamu zaidi na anavyovutia.