Burudani
Meek Mill amchana Drake kwenye wimbo mpya, ugomvi waanza upya
Kama ulijua series ya bifu la Drake na Meek Mill limeisha baada ya ukimya wao wa muda mrefu basi amka kwenye hilo kwasababu Meek Mill amemchana tena Drake kwenye ‘All The Way Up Remix’ akiwa na Fabolous.
Ndani ya wimbo huo Meek Mill amemchana Drake kwa kumwambia, “This is hip-hop, you ain’t write it, don’t record it. I don’t know how they gettin’ down ‘cross the border.”
Mwezi July mwaka jana Nick Minaj ambaye ni mpenzi wa Meek Mill kwa sasa aliwahi kuingilia ugomvi huo kwa kutweet ujumbe uliosema, “fans shouldn’t compare him to Drake because, He don’t write his own raps!”
Hata hivyo Drake aliwahi kumchana Meek Mill kwenye nyimbo zake mbili ‘Charged Up’ and ‘Back to Back’.