Michezo

Mchezaji wa Bournemouth afichua alichoambiwa na Pep Guardiola baada ya mechi

Katika mechi ya ligi kuu ya Uingereza mchezo ulio pigwa jana kati ya Man City na Bournemouth, na Man City waliibuka na ushindi wa goli 2-0 katika uwanja wa Vitality, lakini matokeo ya mechi hiyo hayakuwa mjadala pekee baada ya filimbi ya mwisho, bali maneno ambayo Pep Guardiola alimwambia kiungo Harry Arter yaliwagusa wengi.

Baada ya mechi hiyo kumalizika Pep alienda moja kwa moja kwa kiungo huyo wa Jamhuri ya Ireland, akashika mkono wake ,na kuongea kwa muda mchache, wakaanza kutembea huku kila mmoja akiwa amemuwekea mwenzake mkono.

Baadaye klabu ya Bournemouth wakaweka wazi kuwa Pep alimtakia Arter na mpenzi wake kila la kheri wanapokaribia kupata mtoto.

Arter na mchumba wake, Rachel walipatwa na pigo kubwa Disemba ,2015 kwa kumpoteza mtoto wao wa kike, Renee , wakati akizaliwa. Arter katika mkono wake amejichora ’10-12-2015′, Tattoo hii ni tarehe ambayo mtoto wake Renee alifariki wakati anazaliwa.

“Pole sana kwa kilichotokea, ninakutakia kila la kheri ” hayo ndiyo maneno ya Pep kwa Arter ambaye wiki hii,yeye na mpenzi wake Rachel, wanataraji kupata mtoto
Katika mkutano na waandishi wa habari baada ya mechi Pep alisema ” atakuwa baba hivi karibuni , kwa hiyo nimempa hongera yeye na mpenzi wake kwa sababu ninafahamu kilichotokea siku za nyuma , na ninatumaini mtoto atakuwa salama. “

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents