Burudani
Mchekeshaji wa Afrika Kusini awa mtangazaji wa kipindi cha TV kinachoangaliwa zaidi Marekani ‘Daily Show’
Trevor Noah, mchekeshaji wa Afrika Kusini asiyejulikana kabisa nchini Marekani, amepewa shavu la kuwa mtangazaji wa miongoni mwa vipindi vya TV vinavyoangaliwa zaidi Marekani, Daily Show kinachorushwa kupitia kituo cha Comedy Central kilichokuwa kikishikiliwa na Jon Stewart.
Kituo hicho kinachomilikiwa na kampuni ya Viacom kimedai kuwa kitamtangaza rasmi Noah hivi karibuni.
Mtangazaji wa zamani wa kipindi hicho, Jon Stewart anamkabidhi mikoba Noah
Noah atakuwa mtangazaji wa tatu kuwahi kutangaza kipindi hicho baada ya Craig Kilborn na Stewart.