Burudani
MC Pilipili aweka wazi jina la kitabu chake kipya
Mchekeshaji maarufu Emmanuel ‘MC Pilipili’ Mathias ametaja jina la kitabu chake kitakachozungumzia maisha yake.
MC Pilipili amekiambia kipindi cha The Playlist cha Times FM kuwa kitabu hicho kimegusa sehemu kubwa tatu ikiwemo kutoa burudani, elimu pamoja na tiba ya kisaikolojia.
“Namshukuru Mungu bado hakijakamilika lakini kimefika kurasa zaidi ya 100 sasa hivi. Kila kurasa utafafanua vizuri kabisa kwanini kimeitwa ‘Mtoto wa Nuru’. Mambo matatu makuu tuliyogusa ni pamoja na burudani, elimu na tiba ya kisaikolojia,” amesema.
Mchekeshaji huyo ameongeza kuwa kitabu hiko kimeandikwa na mwandishi maarufu Salum Kim Milongo.