Michezo
Mayweather: Hakuna anayemjua Amir Khan, namtaka Pacquiao
Ushindi wa bondia wa Uingereza, Amir Khan Jumamosi iliyopita dhidi ya Devon Alexander ulimfungulia uwezekano wa kupata pambano alilolisubiri kwa muda mrefu na Floyd Mayweather, lakini Mayweather anasema hana mpango wa kuzichapa na Khan kwa sasa, na kwamba anayemtaka ni Manny Pacquiao tu.
“Usiku uliopita nadhani alipata watu 4,000, hivyo Amir Khan, jina lake halina uzito wowote,” alisema Mayweather.
Amir Khan
“Hakuna anayemjua Amir Khan isipokuwa wale wanaojihusisha na ndondi. Focus yangu ni Manny Pacquiao. Let’s make it happen.”