Habari

Mauaji ya tembo yaiweka Tanzania kwenye kitimoto, magazeti ya UK yamchongea Kikwete kabla ya mkutano wa nchi 50 wiki hii

“Tanzania inaua zaidi ya 11,000 ekwa mwaka kwaajili ya biashara ya pembe za ndovu na Rais wake amefumbia macho ili Prince aje kushikana naye mikono?” limeandika gazeti la Daily Mail la Uingereza.

kikwete

Gazeti hilo limeendelea kuandika kuwa wiki hii Rais Jakaya Kikwete, atakutana na Prince of Wales, Duke of Cambridge, Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron na Rais mambo ya nje wa nchi hiyo, William Hague kwenye mkutano wa viongozi wa nchi 50 huku Tanzania ikiwa na sifa mbaya kwa mauaji ya Tembo.

Mkutano huo ni mahsusi kwaajili ya kuokoa viumbe hao wanaohatarishwa kupotea kutokana na kushamiri kwa mauaji.

Mkutano huo wa Alhamis hii utajaribu kufikia muafaka kuhusiana na muitikio wa kidunia dhidi ya biashara haramu ya pembe za ndovu yenye thamani ya paundi bilioni 6 kwa mwaka na ambayo hudhamini makundi ya kigaidi.

Theluthi ya pembe zote za ndovu zinazokamatwa barani Asia hupitia Tanzania na kila siku tembo 30 huuliwa ambao ni sawa na tembo 11,000 kila mwaka.

“Tanzania is effectively a one-party state with a pervasive intelligence apparatus, and nobody seriously contends that this slaughter is happening without high-level complicity. Yet not a single kingpin has been charged and convicted. MPs, senior officials and businessmen are named in parliament and the media, but investigations fizzle out and little happens,” Daily Mail wameandika.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents