Michezo

Mata aomba radhi baada ya kupata kadi nyekundu

Mchezaji wa timu ya Manchester United, Juan Mata ameomba radhi mashabiki wa timu hiyo baada ya kupata kadi nyekundu kwenye mechi yao dhidi ya West Bromwich Albion.

mata333_1300x1200_2729290a

Mata amepost kwenye akaunti yake ya twitter kwa kusema, baada ya takribani mechi 500, nimetolewa nje ya uwanja kwa ma ya kwanza. Kwenye mchezo huu United walifungwa goli moja kwa bila na West Bromwich Albion, goli ambalo lilifungwa na Rondon dakika ya 66.

mata_2729275a

Mata amesema, “Baada ya mechi takribani 500 kama mchezaji professional, kwa mara ya kwanza nimetolewa nje. Hili ni jipya kwangu lakini tumejifunza. Nimewaumiza sana wachezaji wangu wamecheza wakiwa kumi kwa muda mrefu.”

“Naangalia mechi inayofuata kwa sasa kwenye Europa League dhidi Liverpool. Baada ya kufunga goli pekee dhidi ya Watford nimeongeza uzoefu zaidi,” ameongezea Mata.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents