Michezo
Mashabiki wa Arsenal wamtaka Wenger aondoke
Licha ya ushindi wa magoli manne kwa bila dhidi ya Hull City kwenye mashindano ya kombe la FA, mashabiki wa Arsenal wamtaka Wenger aondoke.
Mashabiki wa Arsenal wameonekana kutofurahishwa na mwenendo wa timu yao baada kufungwa mechi mfululizo ikiwemo ile ya Barcelona, Manchester United, Swansea kabla ya kulazimishwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Spurs wikiendi iliyoisha.
Kitu cha ajabu kwenye mechi hiyo mashabiki wa Arsenal walibeba mabango yaliyoandika, “Arsene, Tunashukuru kwa kumbukumbu zote sasa ni muda wako kusema kwaheri”
Bango lenye maneno kama hayo lilionekana Novemba, 2014 kwenye mechi ya Arsenal walipokuwa ugenini dhidi ya West Bromwich Albion.