Burudani
Marlaw na mkewe Besta wapata mtoto wa pili wa kiume
Mke wa muimbaji Marima “Marlaw” Lawrence, Besta Prosper Rugeiyamu amejifungua mtoto wa pili wa kiume.
Hit maker wa ‘pipi’ Marlaw amepost picha na taarifa njema kwa mashabiki wake kuhusu mke wake kujifungua mtoto wa pili.
Alianza kwa kupost picha ya Besta akiwa na tumbo kubwa la ujauzito na kuandika, “Ni Baraka tu kwa kweli. Tumepata mtoto wa kiume tena.”
Katika picha ya pili waliyopiga wote ameandika “Yaani ni furaha kwa mara nyingine. #BabyBoy. Jina lake moja ni Erence”.
Marlaw na Besta walipata mtoto wa kwanza wa kiume mwishoni mwa mwaka 2013.